Asili Halisi

Micshariki Africa & Adam Shule Kongwe


3:37
#1

 The easy, fast & fun way to learn how to sing: 30DaySinger.com

Jambo woteee...jambo woteee.. Jambo wote..jambo wote

Jambo wote, mtu mzima nshawasili/
Na leo ntaongelea tiba za asili/
Vuteni viti kwanza, shikeni biki kwanza/
Andikeni tiba hii inahusisha mitishamba/
Yani mimea inayotumika kama dawa/
Iwe majani mizizi, maua mbegu na maganda/
Nafaka na gundi na kadhalika/
Pia mpaka matunda yanahusika/
Vilevile makundi ya vyakula mbalimbali/
Hii tiba haihusu dawa zenye kemikali/
Mbali na kukutibu au kukuweka fiti/
Hufanya na kazi ya kujenga mwili/
Na inafanya vyote hivi kwa wakati mmoja/
Hii ndo tiba mama tiba nambari moja/
Asilimia sabini ya waafrika waliitegemea/
Mapinduzi ya kisayansi yalipofika ikalegea/

Ukiangalia gharama ni ndogo au hata bure/
Kachume, kachimbe kunywa na utafune/
Na wala hazidhuru ukiyafuata masharti/
Sasa kimbembe ni kwenye dawa za hospitali/
Mzee... Hizi dawa zina bei/
Yani utateseka sana bila pay/
Mwili ukizizoea unakuwa sugu kwa dawa/
Na ukipona ugonjwa inabaki sumu ya dawa/
Kwa hiyo inakubidi ku recover mara mbili/
Kaa kijanja ndugu kaa kwa akili/
Chunguza kipi kina madhara makubwa/
Upunguze maafa na hasara zitazokuja/
Watafute wajuzi wa tiba hizi/
Sio ushamba jitafute we mswahili/
Usishikiwe akili nature imetubariki/
Imetupa chakula, mimea yenye tiba nyingi/


Wazee wetu walituambia kwamba asili imetimia/
Wao walijifunza na kuitunza miti hiyo/
Ikawatunza pia, wakajitibia magonjwa/
Umwa chochote dawa unayopatiwa unapona/
Tuwaombe watujuze na sisi/
Tujifunze kwa wingi, vyakula na miti/
(yeah) tuache majivuno na ubishi/
(kingine) tubadilishe na mifumo ya kuishi/
Miti mingi tuko nayo mitaani/
(mingi) na mingine wala haiko mbali/
Muhimu kuwa na mashamba na bustani/
Ili isipotee inatupasa kuhifadhi/
Saivi kila kitu dili, naomba nikuhabarishe/
Kuna watu wanatuibia kwa mgongo wa u herbalist/
Epuka wizi huu kwa kusaka maarifa/
Hakikisha na kizazi chako kinarithishwa/

 The easy, fast & fun way to learn how to sing: 30DaySinger.com

Written by: Adam Seleman

Lyrics © DistroKid

Lyrics Licensed & Provided by LyricFind

Discuss the Asili Halisi Lyrics with the community:

0 Comments

    Citation

    Use the citation below to add these lyrics to your bibliography:

    Style:MLAChicagoAPA

    "Asili Halisi Lyrics." Lyrics.com. STANDS4 LLC, 2024. Web. 28 Apr. 2024. <https://www.lyrics.com/lyric-lf/11654326/Micshariki+Africa+%26+Adam+Shule+Kongwe/Asili+Halisi>.

    Missing lyrics by Micshariki Africa & Adam Shule Kongwe?

    Know any other songs by Micshariki Africa & Adam Shule Kongwe? Don't keep it to yourself!

    Browse Lyrics.com

    Quiz

    Are you a music master?

    »
    What song was Kelsea Ballerini famous for?
    A Love Me like You Do
    B Homecoming Queen?
    C The Way It Used to Be
    D Kiss Me More

    Free, no signup required:

    Add to Chrome

    Get instant explanation for any lyrics that hits you anywhere on the web!

    Free, no signup required:

    Add to Firefox

    Get instant explanation for any acronym or abbreviation that hits you anywhere on the web!

    Micshariki Africa & Adam Shule Kongwe tracks

    On Radio Right Now

    Loading...

    Powered by OnRad.io


    Think you know music? Test your MusicIQ here!