Naenda
Micshariki Africa & Adam Shule Kongwe
The easy, fast & fun way to learn how to sing: 30DaySinger.com
Hapo zamani nilikuwa sifaham/ Sikuelewa kabisa mambo ya utoaji dam/ Ukichanganya na story zilizokuwepo mitaa/ Ndo kabisaa, ungeniambia ningeleta balaa/ Ebwana ee, kumbe watu wanakufa/ Afu si tunadanganyana eti damu itauzwa/ Haya mambo ni mazito man/ Usichkulie sio sio sio simple man/ Cheki idadi kubwa ya wahanga wa ajali/ Bado kuna wagonjwa wa upasuaji/ Cheki kina mama wajawazito and/ Wale watoto wenye sickle cell/ Wanahitaji sana damu hata kupita maelezo/ Nasisitiza hata kupita maelezo/ Kila siku, wanahitaji damu ka chakula/ Tena nyingi kwa hiyo inabidi kuwe damu ya dharura/ Sihitaji wa kunishawishi au kukomaa sana/ Najua damu haizalishwi maabara/ Zaidi ya kwa binadamu hakuna pa kuipatia/ Hakuna namna nyingine zaidi ya kuchangia/ Naenda sasa naenda now/ Wenye utayari kama mimi wote naenda nao/ Kuchangia ni hiari naenda kwa hiari yangu/ Naenda kuokoa maisha raia wenzangu/ Nenda sasa nenda now/ Wenye utayari kama wewe wote naenda nao/ Kuchangia ni hiari nenda kwa hiari yako/ Nenda kaokoe maisha raia wenzako/ Naenda leo mi siwezi kukaa tu/ Mwanaume anachangia kila miezi mitatu/ Kina dada kina mama ni miezi minne/ Mtu mwenye vigezo iweje ushindwe/ Hakikisha kwamba umri unaruhusu/ Miaka 18 mpaka 60 au pungufu/ Uzito ni kuanzia kilo 50 kwenda juu/ A donor must have at least 50kgs/ Usiwe mgonjwa wa presha na kisukari/ Usiwe katika tiba hata iwe tiba gani/ Usiwe na magonjwa ya ngozi au kifafa/ Naamini umenielewa of course umenipata/ Kwa mwanamke kuna kitu cha kuongeza/ Usiwe mjamzito au unayenyonyesha/ Kigezo kingine kwa kila mchangiaji/ Asiwe na mwenendo sababishi wa maradhi/ Maradhi hayo ni yale ya kuambukiza/ Mwenendo ni ngono zembe madawa na ulevi pia/ Kuna vigezo vingine nimeviruka?/ Sio kesi watataja nikienda nitavikuta/ Naenda sasa naenda now/ Wenye utayari kama mimi wote naenda nao/ Kuchangia ni hiari naenda kwa hiari yangu/ Naenda kuokoa maisha raia wenzangu/ Nenda sasa nenda now/ Wenye utayari kama wewe wote naenda nao/ Kuchangia ni hiari nenda kwa hiari yako/ Nenda kaokoe maisha raia wenzako/ Ka ni salama kutoa niseme ntaogopa nini/ Watapima vvu kaswende na homa ya ini/ Majibu yanakuwa siri ka uendapo kwa daktari/ Na watacheck mtoaji damu yake kundi gani/ Na kiwango! Lazima kujua ni kitu poa/ Watafuata utaratibu hawafikii kutoa/ Ka umeguswa na unataka ukatoe we shika njia/ Hakuna madhara yoyooote ukichangia/ Ila kwenye faida hapo zipo kedekede/ Yeah, tulia nikuelekeze/ Hupunguza athari ya saratani au cancer/ Hatari ya magonjwa ya moyo na mishipa husepa/ Ukitoa mfululizo kipindi cha miaka sita/ Na kuburn calories pia inakuwa uhakika Kwa kuwa kila muda ukifika unapimwa/ Unaweza kugundua una ugonjwa na ukaanza tiba mapema/ Yote tisa, kumi ndio mwisho kitu ambacho/ Ni kuokoa maisha ya raia wenzako/ Na hujafa hujaumbika bora kuwa mchangiaji/ Huenda kesho ukawa ni wewe au nduguyo anahitaji/ Na kusema damu itauzwa ni uongo wazo chafu/ Hakuna kitu cha thamani kama damu/ Hii damu haiuzwi inagawiwa bure/ Na siku ukihitaji utapatiwa bure/ Na kama ni mchangiaji utapewa kipaumbele/ Pia kumbuka ni hiari uamuzi unao wewe/ Moja/ Na usiseme sijui dini haijaidhinisha/ Kuchangia damu ni zawadi ya maisha/ Na kabla hujasema na mi ni mtu/ Jiulize kama unathamini utu/ Toa damu anza leo acha kusema bado kwanza/ Usingoje matukio au yakitokea mabonanza/ Mi naenda sasa naenda now/ Na wote walio tayari waje niende nao/ Hii ni shule na shule Micshariki
Struggling with Naenda? Become a better singer in 30 days with these videos!
Citation
Use the citation below to add these lyrics to your bibliography:
Style:MLAChicagoAPA
"Naenda Lyrics." Lyrics.com. STANDS4 LLC, 2024. Web. 6 May 2024. <https://www.lyrics.com/lyric-lf/11654379/Micshariki+Africa+%26+Adam+Shule+Kongwe/Naenda>.
Discuss the Naenda Lyrics with the community:
Report Comment
We're doing our best to make sure our content is useful, accurate and safe.
If by any chance you spot an inappropriate comment while navigating through our website please use this form to let us know, and we'll take care of it shortly.
Attachment
You need to be logged in to favorite.
Log In